
Gari la mcheza filamu hot Bongo, Jacqueline Wolper Masawe limefumwa likiwa na kondom za aina mbalimbali.
Ishu hiyo ilidakwa na global publishers, Jumanne ya wiki hii nyakati za mchana wakati msanii huyo akiwa katika mishemishe zake za kila siku.
Mwenyewe alipobanwa kuhusiana na ishu hiyo, alikiri ‘mipira’ hiyo ya kiume ni yake na kwamba, ndiyo silaha kubwa kuliko yoyote hapa duniani, hivyo lazima awe nayo popote.
Staa huyo ambaye kwa sasa yuko kwenye muonekano wa ki-Amber Rose, alikwenda mbele zaidi kwa kuweka wazi kwamba katika ulimwengu huu kondom ni kitu cha kawaida sana.
“Ni bora kutembea na kondom ndani ya gari kuliko pesa kwa sababu ‘zana’ hiyo ndiyo uhai wa mtu na kwa ulimwengu huu ni kitu muhimu.
“Unajua wengi wanaamini pesa ndiyo kitu muhimu, lakini kondom ndiyo silaha bora kuliko zote. Kwa kweli mimi kwenye gari langu lazima ziwepo,” alisema.
Msanii huyo aliongeza kwamba hata kama yupo na ‘mtu wake’ faragha na amesahau ‘kifaa’ hicho, yeye hutoa na kumkabidhi akimwambia: “Baba usipate tabu, kwa vile nakupenda nakulinda.”
Aidha, amewaomba wasanii wenzake (Aunt, Shumileta, Odama, Shamsa Ford na wengine), waige mfano wake kwa kuwa ‘silaha’ hiyo hata kwenye pochi inakaa.
No comments:
Post a Comment